Alhamisi, 5 Mei 2016

DAR ES SALAAM

Meya wa Manispaa ya Kinondoni Bw.BONIFACE JACOB ametangaza kumsimamisha kazi mwanasheria mkuu wa Manispaa hiyo Burton Mahenge na Mthamini wa Manispaa Einhard Chidanga.
Akizungumza na waandishi wa habari amesema wawili hao wameisababishia hasara kubwa na upotevu wa malikatika manispaa hiyo.
Aidha Bw.Jacob amesema wawili hao wameshtakiwa kwa makosa yafuatayo,Mradi wa uwekezaji wa Oysterbay Villa,Mgogoro wa wapangaji wa nyumba za Magomeni kata,Uwekezaji wa eneo la Coco Beach Oysterbay,Mradi wa ujenzi wa maduka ya Makumbusho,Kubomolewa kwa ofisi ya Kata ya Msasani,Ujenzi wa nyumba za Makazi Hiill Road Oysterbay na Ujenzi wa nyumba za makazi Kiwanja Na.314 Toure Drive.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni